Wednesday 11 July 2018

MAJUKUMU YA MWANAMKE DUNIANI

Wanawake duniani wanaonekana kama viumbe dhaifu wasioweza kusimama wenyewe katika kupambana na maisha.Ukitazama majukumu waliyopewa hayawezi kulingana na huo usemi hata siku moja.Mwanamke ana majukumu mengi kwanza ana miliki uzao,chimbuko na pia ni mtawala wa jiko.Ukiyaangalia maneno hayo matatu utaamini kuwa mwanamke anatawala ulimwengu.

Hata shetani anaufahamu ukweli kuwa akimwachia mwanamke apambane katika maendeleo na kumtafuta Mungu basi anaweza kutawala ulimwengu
.Kuna majukumu machache leo nitayataja aliyonayo mwanamke.

  1.  Mwanamke alipewa Neema ya kumzaa Yesu.luka1:26-35
  2. Wanawake walijitoa katika huduma ya Yesu.luka 8:2
  3. Mwanamke alimpaka Yesu mafuta kumuandaa kwa kifo chake.Yoh.12:3
  4. Wanawake walikuwepo msalabani.
  5. Wanawake walikuwa wa kwanza kumuona Yesu alipofufuka.Mathayo28:1-9 
  6. Wanawake wanajali na wanaupendo kuliko wanaume.
  7. Wanawake hujenga nyumba.Mithali 14:1
  8. Wanawake wanaweza kuomba kuliko wanaume.
  9. Mwanamke ni mzazi wa mwanaume
  10. Mwanamke ni mzazi wa kila kilichohai.
Baada ya kuona hayo majukumu machache nadhani wewe mwanamke au mwanaume unayesoma makala hii utaelewa thamani aliyonayo mwanamke.Mwanamke unapaswa kutambua hayo majukumu na kusimama vema kiroho pia katika kupambana na maisha usikubali kurudi nyuma hata kama unapitia magumu katika ndoa yako songa mbele,vumilia kwani wanawake tume pewa upendo na uvumilivu,Kumbuka pia kuwa sisi ndiyo waombaji wazuri na vilio vyetu vinafaida sana katika maombi tuendelee kuwa wanyenyekevu na kuziombea familia zetu.

No comments:

Post a Comment

Toa Weusi Kwa (Pubic Areas) Mapajani na Kwapani Kwa Kutumia Hizi Simple Ingridients

Kuwa na Mapaja meusi au kwapa jeusi kweli ni issue wanayoface wanawake wengi sana so usishangae wala kwasababu ur not alone,mtu unakuwa na ...