Friday 6 July 2018
Zijue faida za karoti kwenye urembo wako
KAROTI zimekuwa zikipatikana msimu mzima wa mwaka na zimekuwa zikiuzwa kwa bei ambayo kila mtu anaimudu. Ni chakula ambacho kina utajiri mkubwa wa vitamini na madini yenye faida nyingi mwilini. Kutokana na utajiri huo karoti sasa imekuwa ikitumika zaidi kwa ajili ya kutengeneza vipodozi vya aina mbalimbali pamoja na sabuni. Ulaji wa karoti au supu yake ni muhimu zaidi katika kutengeneza ngozi kuliko hata kutumia vipodozi kama ilivyo kwa mwili ambapo mwili unaolishwa vizuri ndiyo umekuwa na ngozi nzuri zaidi. Wataalam wa afya wanasema ni bora kula karoti kwa wingi kama unataka kuwa na ngozi yenye muonekano mzuri. Aidha Beta-carotene inayopatikana ndani ya karoti inapoingia mwilini ina uwezo wa kubadilishwa na kuwa vitamin A Aidha kirutubisho cha Fiber kilicho ndani ya karoti ni muhimu kutokana na kukinga kuta za utumbo. Unapotumia karoti mara kwa mara ina uwezo wa kufanya ngozi yako kuwa nzuri na yenye kuvutia. Pia karoti ina asilimia kubwa ya Vitamin C na vitamin D, aidha ina madini Folat, Zink, Madini ya chuma na Calcium Wataalam wa afya wanasema unapokula gramu 50 hadi 75 za karoti kila mara unakuwa umejiwekea kinga dhidi ya magonjwa mbalimbali . Tafiti mbalimbali zilizofanywa zinaonesha karoti zimekuwa na nguvu kubwa ya kukinga watu juu ya kansa ya koo kutokana na vitamini na madini iliyomo ndani yake. juisi ya karoti
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Weusi Kwa (Pubic Areas) Mapajani na Kwapani Kwa Kutumia Hizi Simple Ingridients
Kuwa na Mapaja meusi au kwapa jeusi kweli ni issue wanayoface wanawake wengi sana so usishangae wala kwasababu ur not alone,mtu unakuwa na ...
-
:Kumbe Ukosefu wa Makalio Makubwa Unawafanya Wanawake Wasijikubali Unahisi kwanini
-
huwa tunakuletea Mishono mbalimbali ya nguo,leo tuna mishono ya lace ,vitenge na satin.Naomba kuiita hii peplum new level wengine waita pep...
-
Upo wakati ambapo baadhi ya wasichana huwa hawaridhiki na maumbile yao ya asili, wengine hupenda kuwa wembamba hasa pale mtindo wa maisha...
No comments:
Post a Comment