Sunday 15 July 2018

JINSI YA KUTUNZA NYWELE ZAKO.


Fahamu vyakula vya msingi kwa ajili ya ubora wa nywele zako.

Unaweza Kusuka Mtindo Huu Kwa Kutumia Soft Dread Au Lena
Karibu tena mpenzi msomaji wa makala hii ya Urembo na Mitindo inayokujia kila wiki kupitia safu hii.Katika makala hii nitazungumzia utunzaji wa nywele  kwa wanaume na wanawake .Nitakutajia vyakula ambavyo hufanya nywele kuwa imara  na  zenye mvuto asilia,Watu wengi hulalamika  nywele kukatika,kuwa nyepesi,kuwa kavu na kukosa mvuto.
Watu wengi hupenda kutumia vyakula mbalimbali bila ya kufahamu umuhimu wa vyakula hivyo katika miili yao.Vifuatavyo ni vyakula ambavyo hufanya nywele zako kuwa imara, na vyakula hivi si vigeni katika maisha yetu ya kila siku.



Maharage



Maharage yana protini nyingi kama vile zinc, biotin pamoja na madini ya chuma ambayo hufanya nywele kuwa na virutubisho na muonekano mzuri. Maharage ni mboga inayopendwa na watu wengi, pia ni rahisi kupatikana.  Kadri unavyoitumia ndivyo nywele zako zitakavyozidi kuwa bora na imara zaidi.



Mayai na Maziwa



Watanzania wengi hawana mazoea ya kunywa maziwa huku wengi wakijenga imani potofu kuwa maziwa hufaa kwa watoto wadogo pekee.Maziwa yanaprotini nyingi ambazo husadia kutoa vurutubisho katika nywele na kuzuia kukatika.


Mayai


Mayai pia yanaprotini nyingi ambazo husaidia nywele zako kuwa imara na huzuia  zisikatike hovyo.Hata ukijaribu kuchunguza baadhi ya shampoo ambazo hutumika kusafishia nywele huwa zimetengenezwa kwa mchanganyiko wa kemikali mbalimbali pamoja na mayai.


Samaki



Samaki ni miongoni mwa vyakula muhimu sana katika kustawisha nywele na kuzifanya ziwe imara na zenye muonekano mzuri. Matumizi ya samaki katika mlo husaidia kuzifanya nywele zako kuwa imara toka kwenye ngozi hadi kwenye ncha ya nywele kutokana na uwingi wa protini inayopatikana katika Samaki.


Karoti


Matumizi ya karoti kwa walio wengi hupenda kutumia kama kiugo katika vyakula na hasa mboga.Ni vyema kutumia karoti kwa wingi kwani zina vitamin A na hivyo zitazifanya nywele zako kuwa imara pamoja na kuiacha ngozi yako kuwa yenye kuvutia  na kuondoa ukavu wa ngozi.
Unapotumia karoti inasaidia kuzuia kuungua ngozi wakati unapoweka dawa kichwani, kuepusha michubuko katika ngozi, na pia huzuia kuwepo kwa mba kichwani. Hivyo basi kama unasumbuliwa na mba, ni vyema ukatumia karoti ili kuepukana na tatizo hilo.
Unashauriwa kujua aina yako ya nywele iliuweze kuchagua dawa iliyo sahihi kwa nywele zako hii itakusaidia kuepuka nywele kukatika,kuwa kavu,kuwa nyepesi na kukosa mvuto pia ni muhimu kumtafuta mshauri wa anayejua masawala ya nywele ili uwe na uhakika unapo tumia vupodozi vya nywele.

MWISHO…………


No comments:

Post a Comment

Toa Weusi Kwa (Pubic Areas) Mapajani na Kwapani Kwa Kutumia Hizi Simple Ingridients

Kuwa na Mapaja meusi au kwapa jeusi kweli ni issue wanayoface wanawake wengi sana so usishangae wala kwasababu ur not alone,mtu unakuwa na ...