Friday 8 June 2018

MAPISHI :: PISHI LA NJUGU MAWE NA NAZI PAMOJA NA MAZIWA YA UNGA

Leo tucheki jinsi ya kupika ftari ya njugu mawe ,zinawekwa nazi na maziwa ya unga.
MAHITAJI:-
1. Njugu mawe 1/2
2. Nazi moja
3. Maziwa ya unga vijiko 2- 3 vikubwa
4. Iriki
5. Sukar
6. Custard powder
JINSI YA KUANDAA:-
1. Roweka njugu zako kati ya masaa 2-3
Kisha bandika jikoni ziive ila zisilojeke
2. Kuna Nazi yako na chuja tui la kwanza weka pemben, then tui la pili na tatu weka pemben.
3. Menya hirik yako na ponda mpaka ilainike. Baada ya matayarisho yangu kuwa tayar, naangalia njugu mawe zangu kama zipo tayar, zikiwa zimeiva add tui la pili ulilochuja then acha lichemke na njugu mawe mpaka uone tui lako lipo vizur yaan limeiva. Baada ya hapo chukua maziwa yako ya unga achanganya vizur na maji, kisha changanya pamoja na tui bubu usisahau kuweka kijiko kimoja custard power kijiko kikubwa cha Julia chakula Tizama njugu zako na lile tui la mwanzo litakua limekaa sawa, tia hiriki then malizia tui lako ulilochanganya na maziwa. Pooza mpaka ichemke kisha wacha iive kwa moto kiasi, utaangalia mwenyewe unapenda na lojo jingi au kiac. Kisha epua iftar yangu tayar kwa kuliwa.
mpishi ni Muke Ya Msangi Msangi

No comments:

Post a Comment

Toa Weusi Kwa (Pubic Areas) Mapajani na Kwapani Kwa Kutumia Hizi Simple Ingridients

Kuwa na Mapaja meusi au kwapa jeusi kweli ni issue wanayoface wanawake wengi sana so usishangae wala kwasababu ur not alone,mtu unakuwa na ...