Wednesday 4 July 2018

Utunzaji mgongo ni muhimu



MGONGO  ni moja ya kiungo cha mwili ambacho kinahitaji uangalizi mzuri.Bila hivyo huleta tabu hasa pale mgongo unapokuwa hauko katika muonekano mzuri.
Uchafu unaoganda kwenye mgongo hupelekea muwasho wa mara kwa mara na mgongo kuwa na mabaka mabaka .
Ukweli ni kuwa jaribu kuangalia mgongo wako na kuona kama unastahili kuwa hivyo na kama haustahili basi chukua hatua kwa kuhakikisha mgongo unakuwa msafi na kutafuta tiba ya chunusi au mabakamabaka yaliyo mgongoni mwako.
Unapoufanyia tiba mgongo kwa kutumia sabuni za dawa au lotion utaufanya uwe na muonekano mzuri na hata kuwa huru kuvaa nguo yoyote.
Wengi wanashindwa kuvaa nguo za wazi kutokana na muonekano wa ngozi zao za mgongoni kuwa mbaya zenye vipele, chunusi na kupauka.Madoa kwenye mgongo yamekuwa yakikosesha wengi raha kutokana na suala la utunzaji mgongo halitiliwi maanani kama ilivyo kwenye utunzaji wa uso au miguu.
Tumia brashi laini lenye sababu ya kutosha katika kusugua mgongo wako. Kisha paka mafuta.
Kama huwezi kufikia vizuri mgongo kwa kutumia blashi basi unaweza kuomba msaada ili mradi mgongo  utakate na kuwa katika sura ya kupendeza.
Wengi wanashindwa kuvaa nguo za wazi kutokana na migongo yao kuwa na sura isiyopendeze.
Ni muhimu ukazingatia usafi wa mgongo ili uwe huru kuvaa nguo za wazi bila kuwa na mashaka kuwa kuna watu wanautazama vibaya mgongo wako na wengine wameanza kucheka.


No comments:

Post a Comment

Toa Weusi Kwa (Pubic Areas) Mapajani na Kwapani Kwa Kutumia Hizi Simple Ingridients

Kuwa na Mapaja meusi au kwapa jeusi kweli ni issue wanayoface wanawake wengi sana so usishangae wala kwasababu ur not alone,mtu unakuwa na ...