Monday 28 August 2017

Tumia vipodozi asilia kutunza ngozi yako

Tumia vipodozi asilia kutunza ngozi yako

ulaji wa chakula bora  ni miongoni mwa sababu kuu zinazochangia kuwa na ngozi yenye afya siku zote. Lakini ulaji huo, hufanya kazi vizuri zaidi kwa ndani, hivyo si vibaya na wewe ukafanya jitihada za makusudi katika kuhakikisha ngozi yako inakuwa na muonekano mzuri kwa nje.
Tango ,,Tunda hili linaweza  kupambana na kuchakaa na kuchoka kwa ngozi kunakosababishwa na tabia mbalimbali. Pia  lina uwezo mkubwa wa kusafisha ngozi hasa ya uso. Hiyo ni kazi moja kati ya nyingi zinazofanywa na tunda hili.
Unachotakiwa kufanya ni kusaga tango moja, kisha kuchuja juisi yake. Chukua pamba na chovya kwenye mchanganyiko wako kisha pakaa usoni. Kaa kwa muda wa dakika 20 hadi 30. Osha uso wako, kisha kausha kwa kitambaa safi na laini.Ikiwa juisi itakuwa nyingi, unaweza kuihifadhi kwenye jokofu kwa ajili ya matumizi ya siku za baadaye.


Pendelea kutumia vipodozi vya asili kuwa na ngozi ya asili isiyo na madhara

NAIPENDA NGOZI YANGU YA ASILI

No comments:

Post a Comment

Toa Weusi Kwa (Pubic Areas) Mapajani na Kwapani Kwa Kutumia Hizi Simple Ingridients

Kuwa na Mapaja meusi au kwapa jeusi kweli ni issue wanayoface wanawake wengi sana so usishangae wala kwasababu ur not alone,mtu unakuwa na ...